• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Hai District Council
Hai District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Hai

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dhima na Dira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara
      • Fedha na Biashara
      • Utawala na Utumishi
      • Ardhi na Maliasili
      • Mipango na Takwimu
      • Afya
      • Elimu Msingi
      • Ujenzi
      • Elimu Sekondari
      • Maji
      • Usafi na Mazingira
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
        • Taarifa Idara ya Kilimo
      • Mifugo na Uvuvi
        • Wasilisho Mifugo
      • Maendeleo ya Jamii
    • Vitengo
      • Tehama na Uhusiano
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Nyuki
      • Ugavi na Manunuzi
      • Sheria
      • Uchaguzi
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
      • Maporomoko ya Maji ya Nshara
      • Chemchemi ya Chemka
      • Mila na Utamaduni
      • Uwanja wa Ndege wa Kimataifa
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Industry and Trade
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Maji
    • Huduma za Elimu
    • Kilimo
    • Huduma za Watumishi
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Kamati ya Fedha, Uongozi na Mipango
      • Kamati ya Elimu, Afya na Maji
      • Kamati ya UKIMWI
      • Kamati ya Maadili
    • Ratiba ya Vikao vya Madiwani
    • Ratiba ya Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi Mipya
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Fomu
      • Ahadi ya Uadilifu kwa Viongozi
      • Ahadi ya Uadilifu Watumishi
      • Fomu ya Maombi ya Likizo
      • OPRAS Walimu
      • OPRAS Watumishi
    • Miongozo
    • Taarifa
    • Sheria Ndogo
  • Kituo cha Habari
    • Maktaba ya Video
    • Maktaba ya Picha
    • Matukio
    • Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
      • Taarifa kwa Umma-Mikopo
    • Jarida
  • Mifumo
    • Mfumo wa Kiuhasibu (FFARS)
    • Mfumo wa Bajeti (Planrep)
    • Mfumo wa Vibali Safari za Nje
    • Mfumo wa Taarifa za Mapato (LGRCD)
    • Mfumo wa Taarifa za Shule (TanzaniaSIS)
    • Usajili Kupata TIN (TRA)

Wanawake, Vijana jiungeni kwenye vikundi mnufaike na mikopo ya Serikali: Diwani Masama Kusini

Imetumwa: January 21st, 2021




Diwani wa Kata ya Masama Kusini Cedrick Pangani, amewashauri Wanawake, Vijana na Watu wenye ulemavu kuendelea kujiunga kwenye vikundi ili waweze kufikiwa kwa urahisi kwenye mikopo inayotolewa na hamlashauri ili fedha hizo ziweze kusaidia kuwainua kiuchumi.

 

Hayo ameyasema leo Januari 20 mwaka 2021 wakati wa ziara yake ya kuvitembelea vikundi vilivyopo ndani ya kata yake ambavyo vinanufaika na asilimia 10 ya mapato ya ndani yanayotolewa na halmashauri ya Wilaya ya Hai.

 

Akizungumza na Kikundi cha Wajane, Wagane na Wapweke (WANA WA ASAFU), kilichopo chini ya Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Ushirika wa Makuna Mtaa wa Majengo wilayani humo, Diwani Pangani amewataka Wanawake Vijana na Watu wenye ulemavu ili waweze kunufaika na mikopo hiyo.

 

Amesema vipo vikundi vingi vimekuwa vikipata mikopo, lakini havina elimu ya kutosha ya namna ambavyo vinaweza kuitumia kikopo hiyo kwa ajili ya kuendesha miradi ya kiuchumi.

 

“Naomba nitoe wito kwa wanufaika wa mikopo hii kuhakikisha kwamba fedha wanazopewa zinakwenda kutekeleza miradi au biashara walizokusidia na kujenga tabia ya kuzirejesha kwa wakati ili ziweze kunufaisha vikundi vingi zaidi kama inavyotarajiwa,”amesema.

 

Amesema ziara hiyo imelenga kukutana na vikundi ambavyo vinanufaika na asilimia 10 ya mapato ya ndani yanayokusanywa na halmashauri ya Hai, hivyo nimeamua kuvitembelea vikundi hivi kwani kuna vingine havijui namna ya kuomba mikopo hiyo na vikundi vingine vimekuwa vinapata mikopo hiyo lakini havina elimu yakutosha.

 

“Katika ziara yangu hii nimelazimika kumbatana na Wataalam wa Maendeleo ya Jamii wa Kata, ili kuvipitia vikundi vyote vilivyonufaika na mikopo hii ili kuwaelimisha na kuwasikiliza changamoto wanazokumbana nazo,”amesema.

 

Kwa upande wake Afisa Maendeleo ya Jamii Kata ya Masama Kusini Bi. Lilian Loth, amesema vikundi vingi vilivyopo katika kata hiyo havipendi kusajiliwa kwa kuhofia kupoteza muda wao wa kuzalisha mali na kukaa kwa ajili ya kutengeneza Katiba.

 

“Katika kata yangu vipo vikundi vingi havijasajiliwa, vikundi vilivyosajiliwa hadi sasa ni vikundi 18 tu, lakini kuna vikundi vingine vinapoomba mkopo na kiushindwa kupata vimekuwa vikikata tamaa ya kuomba mkopo hali ambayo inapelekea kujiondoa kwenye vikundi vya ujasiriamali,’amesema Bi. Loth.

 

Naye Mwenyekiti wa Kikundi cha Wajane, Wagane na Wapweke Bi. Jane Massawe, amesema vikundi vingi havijapata elimu ya kuomba mikopo kutoka halmashauri na kuiomba serikali kutupitia kwa maafisa Maendeleo ya Jamii kuvitembelea vikundi viliuvyopo vijijini ili viweze kupata elimu hiyo ya mikopo.

 

Katibu wa kikundi hicho Elisamia Munis, amesema ni vema kabla vikundi hivyo havijapewa mikopo ni vyema vikapatiwa elimu vikundi vingi vimekuwa vikikimbilia kuomba mikopo lakini hawana mradi ambao wanakwenda kuufanya jambo ambalo limekuwa likipelekea kushindwa kuirudisha mikopo hiyo.

 


Matangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI UCHAGUZI MKUU 2020 October 10, 2020
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI UCHAGUZI MKUU 2020 October 10, 2020
  • TANGAZO LA USIMAMIZI WA VITUO VYA KUPIGIA KURA KATIKA UCHAGUZI MKUU WA RAIS, WABUNGE NA MADIWANI MWAKA 2020 October 20, 2020
  • Vitambulisho vya Wajasiriamali Wadogo 2020 May 30, 2020
  • Ona Yote

Habari Mpya

  • Madiwani Kushiriki Kutokomeza Rumbesa Wilaya ya Hai

    February 24, 2021
  • Serikali Kuwakamata Wasiodai na Wasiotoa Risiti za Biashara

    February 17, 2021
  • DCC Yaishauri Halmashauri ya Hai Kuimarisha Vyanzo vya Mapato

    February 16, 2021
  • Mkurugenzi Sintoo Ahimiza Matumizi Sahihi Fedha na Muda Kutekeleza Miradi ya Maendeleo

    February 15, 2021
  • Ona Yote

Video

Wilaya ya Hai Nafasi ya 4 Kitaifa Darasa la Saba 2020
Vidio Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Planrep
  • TANEPS
  • Mfumo wa Ajira za Afya
  • Blog ya Wilaya
  • Fomu ya Maombi ya Likizo
  • Fomu ya OPRAS - Walimu
  • Fomu ya OPRAS - Watumishi
  • Matokeo ya Mtihani wa Darasa la Saba Shule za Wilaya ya Hai Mwaka 2020
  • Muundo wa Halmashauri

Viunganishi Vinavyohusiana

  • Mamlaka ya Serikali Mtandao
  • Utumishi
  • Tovuti kuu ya serikali
  • TAMISEMI
  • Mfumo wa Bajeti
  • Mfumo wa Vibali vya Kusafiri nje ya nchi

Watembeleaji Duniani

world map hits counter

Idadi ya Watembeleaji

free HitCounter

Ramani

Wasiliana Nasi

    Kitongoji cha Bomani

    Anuani ya Posta: 27 Hai

    Simu: 0272758441

    Simu ya Mkononi: 0752195133

    Barua Pepe: ded@haidc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani
    • Huduma

Hatimiliki © 2017 Halmashauri ya Wilaya ya Hai