• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Hai District Council
Hai District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Hai

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dhima na Dira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara
      • Fedha na Biashara
      • Utawala na Utumishi
      • Ardhi na Maliasili
      • Mipango na Takwimu
      • Afya
      • Elimu Msingi
      • Ujenzi
      • Elimu Sekondari
      • Maji
      • Usafi na Mazingira
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
        • Taarifa Idara ya Kilimo
      • Mifugo na Uvuvi
        • Wasilisho Mifugo
      • Maendeleo ya Jamii
    • Vitengo
      • Tehama na Uhusiano
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Nyuki
      • Ugavi na Manunuzi
      • Sheria
      • Uchaguzi
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
      • Maporomoko ya Maji ya Nshara
      • Chemchemi ya Chemka
      • Mila na Utamaduni
      • Uwanja wa Ndege wa Kimataifa
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Industry and Trade
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Maji
    • Huduma za Elimu
    • Kilimo
    • Huduma za Watumishi
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Kamati ya Fedha, Uongozi na Mipango
      • Kamati ya Elimu, Afya na Maji
      • Kamati ya UKIMWI
      • Kamati ya Maadili
    • Ratiba ya Vikao vya Madiwani
    • Ratiba ya Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi Mipya
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Fomu
      • Ahadi ya Uadilifu kwa Viongozi
      • Ahadi ya Uadilifu Watumishi
      • Fomu ya Maombi ya Likizo
      • OPRAS Walimu
      • OPRAS Watumishi
    • Miongozo
    • Taarifa
    • Sheria Ndogo
  • Kituo cha Habari
    • Maktaba ya Video
    • Maktaba ya Picha
    • Matukio
    • Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
      • Taarifa kwa Umma-Mikopo
    • Jarida
  • Mifumo
    • Mfumo wa Kiuhasibu (FFARS)
    • Mfumo wa Bajeti (Planrep)
    • Mfumo wa Vibali Safari za Nje
    • Mfumo wa Taarifa za Mapato (LGRCD)
    • Mfumo wa Taarifa za Shule (TanzaniaSIS)
    • Usajili Kupata TIN (TRA)

Wananchi Watakiwa Kumuenzi Nyerere kwa Vitendo

Imetumwa: October 14th, 2020

Wito umetolewa kwa watanzania kumuenzi kwa vitendo Hayati Baba wa Taifa Mwalimu Julius Nyerere kwa kufanya mambo ambayo aliyasimamia na kuyaamini kuwa yataleta maendeleo kwa Taifa.

Akimuwakilisha Mkuu wa Wilaya ya Hai kwenye maadhimisho ya Siku ya Vijana na Kumbukizi ya Baba wa Taifa; Afisa Tarafa wa Masama Nsajigwa Ndagile amesema ni wajibu wa wananchi wote kila mmoja kwa eneo lake kufanya kazi ili kufanikisha maono ya Mwalimu Nyerere kwa Taifa la Tanzania.

Nsajigwa amesema kuwa Nyerere aliamini kwamba kufanya kazi kwa bidi kutaondoa utegemezi wa mtu mmoja mmoja na hatimaye kwa nchi nzima na kwamba kazi ndiyo msingi wa maendeleo.

Ameongeza kuwa Baba wa Taifa alianzisha mapambano dhidi ya maadui ujinga, maradhi na umasikini pamoja na rushwa aliyoitambulisha kama adui wa haki na maendeleo; na kuwataka wananchi kuendeleza mapambano hayo kwa manufaa ya nchi yao.

“Leo hatumkumbuki Mwalimu Nyerere kwa sababu ya idadi ya nyumba au magari aliyomiliki bali kwa sababu ya mchango wake katika maendeleo ya nchi hii” ameongeza Nsajigwa.

Aidha Nsajigwa ametumia jukwaa hilo kuipongeza Halmashauri ya Wilaya ya Hai kwa namna inavyochangia kuinua vijana kiuchumi kwa kuwapatia mikopo, kuwakutanisha na elimu ya ujasiriamali na namna ya kupata masoko ya bidhaa zao.

Kwa upande wake Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Hai Yohana Sintoo, amesema halmashauri yake itaendelea kutoa mikopo kwa vijana na makundi mengine ya wanawake na watu wenye ulemavu ili kuwainua kiuchumi.

Katika kuelekea Uchaguzi Mkuu wa Rais, Wabunge na Madiwani; Sintoo amewataka wananchi kujitokeza kusikiliza sera za wagombea ili kujiongezea uelewa wa kufanya maamuzi sahihi ya kuchagua kiongozi anayefaa siku ya kupiga kura.

Sintoo ametumia maadhimisho hayo kucheza moja ya hotuba za Mwalimu Nyerere inayowakumbusha wananchi kuwaepuka wagombea wanaowashawishi kuwachagua kwa misingi ya ukabila na Imani za kidini.

Halmashauri ya Wilaya ya Hai imefanya maadhimisho ya Kilele cha Wiki ya Vijana na Kumbukizi ya Kifo cha Baba wa Taifa kwa kufanya mdahalo wa wanafunzi, maonesho ya kazi za vijana katika ubunifu, Sanaa, biashara na ujasiriamali pamoja na hotuba za viongozi.

Matangazo

  • TANGAZO LA UKUSANYAJI NA UZOAJI TAKA HAI MJINI September 27, 2023
  • MATOKEO YA MTIHANI WA DARASA LA SABA (PSLE) 2023 WILAYA YA HAI November 23, 2023
  • MAJINA YA WALIOITWA USAHILI NAFASI ZA JESHI WILAYA YA HAI September 06, 2023
  • TANGAZO LA UKUSANYAJI NA UZOAJI TAKA HAI MJINI September 27, 2023
  • Ona Yote

Habari Mpya

  • Mhe Kaijage Awataka Watumishi Kufanya Kazi Kwa Bidii

    November 22, 2023
  • Mkalipa Ataka Viongozi Wa Dini Kufundisha Waumini

    November 08, 2023
  • Wananchi wa Kijiji cha Sanya Station Washukuru Ulipwaji Wa Fidia

    October 25, 2023
  • Mkurugenzi Dionis Myinga Aishukuru Kambele Kwa Msaada Wa Sementi

    October 23, 2023
  • Ona Yote

Video

UGAWAJI WA PIKIPIKI WILAYA YA HAI
Vidio Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Planrep
  • TANEPS
  • Mfumo wa Ajira za Afya
  • Blog ya Wilaya
  • Fomu ya Maombi ya Likizo
  • Fomu ya OPRAS - Walimu
  • Fomu ya OPRAS - Watumishi
  • Matokeo ya Mtihani wa Darasa la Saba Shule za Wilaya ya Hai Mwaka 2020
  • Muundo wa Halmashauri

Viunganishi Vinavyohusiana

  • BARUA PEPE YA MALALAMIKO
  • Mamlaka ya Serikali Mtandao
  • Utumishi
  • Tovuti kuu ya serikali
  • TAMISEMI
  • Mfumo wa Bajeti

Watembeleaji Duniani

world map hits counter

Idadi ya Watembeleaji

free HitCounter

Ramani

Wasiliana Nasi

    Kitongoji cha Bomani

    Anuani ya Posta: 27 Hai

    Simu: 0272758441

    Simu ya Mkononi:

    Barua Pepe: ded@haidc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani
    • Huduma

Hatimiliki © 2017 Halmashauri ya Wilaya ya Hai