Kamati ya Maendeleo ya Kata ya Muungano imefanya kikao cha kawaida cha kupokea na kujadili taarifa ya utekelezaji wa shughuli za maendeleo kwa robo ya pili ya mwaka katika kata hiyo.
Katika kikao hicho kilichofanyika Januari 26,2027 katika shule ya msingi Kambi ya Raha ,kamati imemshukuru Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt Samia Suluh Hassan kwa kuipatia kata hiyo fedha kwa ajili ya ujenzi wa madarasa mapya matatu katika shule ya msingi Kambi ya Raha, pamoja na ujenzi wa mashimo sita ya vyoo, mradi wenye thamani ya shilingi milioni 88.2.
Aidha, kikao hicho kimepongeza juhudi za kukamilisha ujenzi wa madarasa mawili kwa gharama ya shilingi milioni 25, yaliyojengwa kwa nguvu za wananchi kwa kushirikiana na diwani wa Kata ya Muungano, Edmund Rutaraka.
Kamati hiyo pia imemshukuru Mbunge wa Jimbo la Hai Saashisha Mafuwe kwa mchango wa fedha uliotolewa kusaidia ukamilishaji wa madarasa hayo, hatua inayolenga kuboresha mazingira ya elimu katika kata hiyo.
Kitongoji cha Bomani
Anuani ya Posta: 3 RD TTCL RC CHURCH 25382, P.O BOX 27 Hai
Simu: 0754553560
Simu ya Mkononi: 0754553560
Barua Pepe: ded@haidc.go.tz
Hatimiliki © 2017 Halmashauri ya Wilaya ya Hai