Hatua Muhimu za kupata Kibali cha Kusafirisha Mazao ya Misitu
Kibali cha kusafirisha mazao ya misitu kinatolewa na Wakala wa Misitu Tanzania TFS (Tanzania Forest Service)
Mteja aliye ndani ya Wilaya ya Hai anatakiwa kuandika barua ya kuomba kibali Ofisi ya Mkurugenzi Mtendaji Halmashauri ya Wilaya ya Hai, na barua hiyo inatakiwa kupitia kwa Mtendaji wako wa Kijiji ili Mtendaji huyo athibitishe ombi lako. Pia barua ya maombi lazima iambatanishwe na kibali cha Mteja alichopewa kuvuna zao la misitu husika.
Wataalam wa Misitu Ofisi ya Mkurugenzi Mtendaji watatembelea na kufanya ukaguzi ili kujiridhisha kuhusu zao la misitu linalotakiwa kusafirishwa.
Wataalam wakiridhika na ombi la Mteja,basi mteja atalazimika kulipia ushuru wa asilimia 5 ya bei ya kununua au kuuza; ushuru huu utalipwa kwa halmashauri ya Hai na Mteja anatakiwa kupatiwa Risiti
Baada ya Mteja kufanya malipo ya Ushuru kwa Halmashauri, kibali cha kusafirisha zao la misitu kitatolewa kutoka TFS.
Kibali kitakachotolewa kitatumika ndani ya muda maalumu tangu tarehe ya kutolewa. Mteja anashauriwa kutoa taarifa ofisi aliyopata kibali au ofisi ya karibu iwapo atapata tatizo la kukwamisha kusafirisha mzigo wake kwa muda uliowekwa ili kupata msaada zaidi.
Iwapo Mteja hajatoa taarifa yoyote ndani ya siku tatu, kibali hicho kitakuwa hakitumiki tena na mteja huyo atalazimika kuomba tena kibali kingine.